IQNA

Mbunge wa kwanza Muislamu aingia katika bunge la Australia

16:33 - August 24, 2010
Habari ID: 1980504
Ed Husiç amekuwa mbunge wa kwanza Muislamu nchini Australia baada ya kupata kura nyingi zaidi katika eneo la Sydney.
Mtandao wa webhaber umeripoti kuwa Ed Husiç ambaye ni mwanachama wa chama cha Leba cha Australia na Muislamu mwenye asili ya Bosnia amefanikiwa kupata kura nyingi za kiti cha binge katika mji wa Sydney.
Hadi sasa hakuna Muislamu aliyewahi kuwa mbunge nchini Australia na ushindi wa Ed Husiç umeyafurahisha mno makundi ya Kiislamu nchini humo.
Waislamu wanaishi nchini Australia kwa zaidi ya miaka 200 na idadi yao inafikia watu milioni moja. Waislamu wengi wa Australia wanaishi katika miji ya Melborn na Sydney.
Idadi ya misikiti, nyumba za ibada na shule za Kiislamu barani Australia ni kati ya 300 hadi 350. 640603


captcha