Kwa mujibu wa kituo cha habari cha Muhit, hati hiyo imechapishwa baada ya kuhakikisha kwamba inaoana kikamilifu na misingi ya mafundisho ya Kiislamu, Qur'ani Tukufu na Hadithi za Mtume (saw).
Hati hiyo inajumuisha haki za Kiislamu, kijamii na kibinadamu za watoto zilizochunguzwa na kuchambuliwa na wanafikra za Kiislamu na kueleza mjadala wa harakati za kijamii za watoto.
Kamati ya Kimataifa ya Kiislamu ya Mwanamke na Mtoto itatuma hati hiyo katika Jumuiya ya Nchi za Kiislamu OIC kwa ajili ya kupasishwa na kutambuliwa rasmi kuwa marejeo ya shughuli zinazohusiana na masuala ya watoto ndani na nje ya ulimwengu wa Kiislamu hususan katika duru za kimataifa. 661588