IQNA

Kikao cha 'Uadilifu, Amani' chafanyika Canada

17:23 - October 30, 2010
Habari ID: 2022237
Kikao cha tatu cha Jukwaa la Kiislamu la Amani Kimataifa kimefanyika huko Ottawa Canada chini ya anwani ya 'Amani Yenye Uadilifu, Mazungumzo ya Pamoja Duniani.'
Kongamano hilo limejadili masuala kuhusu fikra za kidini, tamaduni na amani kwa mtazamo wa Kiislamu na juhudi za kuleta amani duniani. Aidha washiriki wamejadili masuala kama vile ugaidi, umasikini, ubaguzi wa rangi na ukosefu wa uadilifu.
Kwa mujibu wa IQNA, kongamano hilo limehudhuriwa na washiriki kutoka Venezuela, Marekani, Canada na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
Washiriki kutoka Iran walikuwa ni pamoja na Saeed Ameli wa Chuo Kikuu cha Tehran na mbunge wa zamani Elham Aminzadeh.
684479
captcha