IQNA

Kikao cha Uislamu na Uchumi kufanyika Uturuki

21:17 - December 04, 2010
Habari ID: 2042061
Kikao cha tatu cha Uislamu na Uchumi kimepangwa kufanyika tarehe 11 Disemba katika mji wa Istanbul nchini Uturuki kikisimamiwa na Jumuiya ya Wachumi wa nchi hiyo.
Kituo cha habari cha Dunyabulteni kimetangaza kuwa kikao hicho kitahudhuriwa na wataalamu wa masuala ya uchumi, wahadhiri wa vyuo vikuu na wawakilishi wa bunge la Uturuki.
Miongoni mwa maudhui zitakazojadiliwa katika kikao hicho ni mazungumzo kuhusu benki na mfumo wa fedha wa Kiislamu, uongozi wa Kiislamu, siasa za kijamii katika Uislamu na bima na biashara katika sheria za Kiislamu. 705988

captcha