Kwa mujibu wa mwandishi wa IQNA, maombolezo hayo yanafanyika katika Shule ya Uthmaniya kaunzia Disemba 7 na yataendelea hadi siku ya Ashura, tarehe 10 Muharram.
Majlisi hizo zimeandaliwa na Jumuiya ya Uthmaniya katika eneo la Zangipur.
Sarafraz Ahmad aliyesoma katika Chuo Kikuu cha Baghdad anatoa mihadhara yenye anuani ya 'Tunayojifunza katika Maisha ya Mtume SAW".
Waislamu wa madhehebu ya suni nchini India hufunga saumu katika siku ya Ashura kama njia ya kufungamana na subira ya Imam Hussein AS na familia za mashahidi wa Karbala.
708630