IQNA

Mpango wa Kiislamu wa kuwalisha maskini sikukuu za Krismasi waanza

16:40 - December 25, 2010
Habari ID: 2052979
Kituo cha Kiislamu cha Oklahoma City nchini Marekani kikishirikiana na jumuiya nyingine mbili za Kiislamu kimeanza kutekeleza mpango wa kuwapa chakula watu wasiokuwa na makazi katika siku za sherehe za Krismasi.
Kituo cha habari cha NEWSOK kimeripoti kuwa Kituo cha Kiislamu cha Msikiti wa Oklahoma City kimeanza kutekeleza mpango huo adhuhuri ya leo Jumamosi.
Mpango huo wa kuwapa chakula watu wasiokuwa na makazi katika sikukuu za Krismasi unatekelezwa kwa ushirikiano wa Baraza la Kiislamu la Oklahoma City na Baraza la Uhusiano wa Kiislamu na Marekani tawi la Oklahoma.
Mwenyekiti wa Kituo cha Kiislamu cha Oklahoma Imad Anchasi amesema kuwa dini ya Kiislamu inatufunza kuwasaidia watu wasiojiweza.
Msemaji wa kituo hicho Saad Muhammad pia amesema, kwa mujibu wa mpango huo, watu wasiojiweza wametayarishiwa usafiri wa kuwapeleka katika msikiti wa mji huo, na mbali na chakula watapewa zawadi ya blanketi.
Amesema kuwa sikukuu ya Krismasi ni wakati muafaka wa kutoa chakula kwa watu wasioweza kumudu gharama za maisha yao. 717449

captcha