Gazeti la al Rai linalochapishwa Kuwait limeandika kuwa Mkuu wa Kamati ya Habari ya mashindano hayo Ali al Awadhi amesema pendekezo hilo limetolewa baada ya vikao kadhaa vya mashauriano na taasisi husika wakiwemo maafisa wa Wizara ya Wakfu na Masuala ya Kiislamu.
Amesema maamuzi yaliyochukuliwa yamewasilishwa kwenye kamati ya masuala ya fedha.
Ali al Awadhi ameongeza kuwa katika vikao hivyo kumetolewa mapendekezo mengi ikiwa ni pamoja na kuainisha kipimo cha kiwango cha mafanikio ya mashindano hayo. 739546