Ripoti zinasema kuwa jumuiya zinazowaunga mkono Wapalestina hususan kundi la Mshikamano na Mapambano katika Ulimwengu wa Kiarabu, yametoa taarifa mbalimbali yakiwataka Waislamu na wasiokuwa Waislamu kuandamana siku ya tarehe 15 Mei katika miji mbalimbali kwa ajili ya kupinga uvamizi wa Wazayuni dhidi ya ardhi ya Palestina.
Taarifa ya kundi la Mshikamano na Mapambano ya Ulimwengu wa Kiarabu imesema kuwa tarehe 15 Mei mwaka huu inapaswa kupewa jina la Siku yaa Palestina katika harakati za mapambano ya ulimwengu wa Kiarabu na walimwengu wote wanapaswa kukwamisha malengo ya utawala ghasibu wa Israel.
Taarifa hiyo imesema kuwa wananchi wa Paris watakutana saa tisa jioni katika Medani ya Jamhuri kwa ajili ya kuwaunga mkono na kuwatetea wananchi wanaokandamizwa wa Palestina.
Baadhi ya wakimbizi wa Kipalestina watasimulia masaibu yaliyowapata kutoka kwa askari wa utawala ghasibu wa Israel. 790867