IQNA

Bunge la Bulgaria lalaani shambulizi dhidi ya msikiti

19:40 - May 28, 2011
Habari ID: 2129750
Bunge la Bulgaria limetoa taarifa likilaani shambulizi lililofanywa na wafuasi wa chama chenye misimamo mikali cha Ataka dhidi ya msikiti wa Banya Bashi mjini Sofia.
Taarifa hiyo kali ya wabunge wa Bulgaria imekemea na kulaani mashambulizi yaliyofanywa na wafuasi wa chama cha Ataka dhidi ya Waislamu waliokuwa wakitekeleza ibada katika msikiti huo.
Taarifa hiyo imesema shambulizi hilo ambalo limefanyika dhidi ya Waislamu waliokuwa wakitekeleza ibada siku ya Ijumaa ni hatua ya kuaibisha ambayo haiwezi kufumbiwa macho.
Sehemu nyingine ya taarifa ya bunge la Bulgaria imesema kitendo hicho kitatayarisha mazingira ya kutokea mivutano na ghasia za kidini na imetahadharisha juu ya matokeo yake mabaya.
Shambulizi la wafuasi wenye misimamo mikali wa chama cha Ataka dhidi ya msikiti wa Banya Bashi limesababisha mgawanyiko ndani ya chama hicho chenyewe na kuwafanya baadhi ya wawakilishi wake bunge kujitenga. 799317

captcha