IQNA

Zaidi ya misikiti 100 kujengwa Imarati

0:55 - June 29, 2011
Habari ID: 2146156
Idara ya Wakfu na Masuala ya Kheri ya Imarati (GAIAE) imetangaza kuwa itajenga karibu misikiti 140 nchini humo hadi kufikia mwishoni mwa mwaka huu.
Shirika la habari la Imarati WAM limeripoti kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Idara ya Waqfu na Masuala ya Kheri ya nchi hiyo Muhammad Abid al Mazrui amesema misikiti hiyo mipya itajengwa kwa lengo ya kuboresha hali ya watu wanaokwenda kutekeleza ibada ya swala.
Amesema misikiti 8 itajengwa katika eneo la Bani Yas, 16 katika eneo la Magharibi, 8 huko al Ain, 20 Sharja, 18 Ajman, 12 Fujaira, 9 katika eneo la Umm al Qaiwin, 27 Raasul Khaima, na 8 katika eneo la Khur Fakan.
Ameongeza kuwa msikiti mmoja wa Fujaira na mingine 9 ya Raasul Khaima itakarabatiwa. 816686



captcha