IQNA

Duru ya pili ya mafunzo ya muda ya maarifa ya Ahlul Bait (as) kutolewa Mali

15:33 - July 19, 2011
Habari ID: 2156496
Duru ya pili ya masomo ya muda kuhusu elimu na maarifa ya Ahlul Bait (as) itaanza tarehe 21 Julai katika mji wa Sikaso katika Jamhuri ya Mali. Masomo hayo yanasimamiwa na Jumuiya Kuu ya Ahlul Bait ya Mali.
Masomo hayo yatawashirikisha walimu wa lugha za Kiarabu na Kifaransa wa mji wa Sikaso na yataendelea kwa kipindi cha siku tatu.
Hujjatul Islam Walmuslimin Ibrahim Samaki mwakilishi wa Kitengo cha Utamaduni cha Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika eneo la Sikaso nchini Mali amesema masomo mengine kama hayo yatatolewa nchini kote Mali kabla kidogo ya kuanza mwezi mtukufu wa Ramadhani.
Walimu 40 wa lugha za Kiarabu na Kifaransa wa eneo la Sikaso watashiriki katika mafunzo elimu na maarifa ya Ahlul Bait (as). Duru ya kwanza ya mafunzo hayo ilifanyika mwaka jana chini ya usimamizi wa Kituo cha Utamaduni cha Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nchini Mali. 827668
captcha