IQNA

Ayatullah Bashir Najafi:

Ufaransa inapaswa kutazama upya marufuku ya hijabu

14:24 - July 20, 2011
Habari ID: 2157146
Ayatullahil Udhma Bashir Hussein Najafi ambaye ni miongoni mwa maulamaa wakubwa wa Iraq ameitaja serikali ya Ufaransa kutazama upya sheria ya marufuku ya vazi ya stara la mwanamke wa Kiislamu hijabu katika shule na ofisi za serikali.
Ayatullah Najafi alitoa matamshi hayo jana mjini Najaf katika mazungumzo yake na balozi wa Ufaransa nchini Iraq Bwana Denis Gauer. Ameitaka Ufaransa kutazama upya sheria hiyo inayowazuia wanawake wa Kiislamu kuingia mashuleni au katika ofisi za serikali ya nchi hiyo wakiwa na vazi la hijabu.
Sheikh Ali Najafi msemaji wa Ayatullahil Udhma Bashir Najafi amesema kuwa mazungumzo kati ya mwanazuoni huyo mkubwa na balozi wa Ufaransa nchini Iraq yaliendelea kwa kipindi cha saa nzima na kwamba pande hizo mbili zimejadili masuala yanayohusiana na Iraq, biashara na uchumi wa nchi hizo mbili. Amesema pande hizo pia zilijadili marufuku ya hijabu ya Kiislamu nchini Ufaransa na udharura wa kufutwa marufuku hiyo ambayo ni kinyume na demokrasia ya nchi za Magharibi inayoruhusu uhuru wa mtu binafsi. 827977

captcha