IQNA

CAIR yawaalika wasiokuwa Waislamu misikitini huko Marekani

20:35 - July 20, 2011
Habari ID: 2157269
Baraza la Uhusiano wa Kiislamu na Marekani (CAIR) limewataka viongozi wa misikiti nchini Marekani kufungua milango ya vituo vya ibada kwa ajili ya wasiokuwa Waislamu katika mwezi mtukufu wa Ramadhani.
CAIR imesema kuwa mazungumzo kati ya Waislamu na wasiokuwa Waislamu ndiyo njia bora zaidi ya kukabiliana na ongezeko la hujuma ya propaganda chafu dhidi ya Uislamu na Waislamu duniani na limewataka wasimamizi wa misikiti wafungue wazi milango ya vituo vya ibada kwa ajili ya wasiokuwa Wislamu katika mwezi ujao wa Ramadhani.
Sehemu moja ya taarifa ya CAIR imesema watu wasiokuwa Waislamu ambao wanasuhubiana na Waislamu wana mitazamo ya wastani kuhusu dini ya Kiislamu na kwa kawaida huwa hawatoi maoni yasiyokuwa na maana kuhusu dini hiyo.
Taarifa hiyo imesema kuwepo Wasiokuwa Waislamu katika chakula cha futari ya mwezi mtukufu wa Ramadhani misikitini ndiyo njia bora zaidi ya mazungumzo kati ya watu hao na Waislamu na njia muafaka ya kukabiliana na propaganda za kuwatisha watu kuhusu dini ya Kiislamu. 828604
captcha