Masomo hayo ambayo ni makhsusi kwa walimu wa malezi ya Kiislamu yataendelea kwa kipindi cha miezi saba.
Mkurugenzi wa Idara ya Masuala ya Wanawake katika Wizara ya Wakfu na Masuala ya Kidini ya Palestina Maisara al Naubani amesema kuwa masomo hayo yanasimamiwa na wizara hiyo kwa lengo la kuboresha kiwango cha kiraa na tajwidi ya Qur'ani Tukufu katika jamii na kuimarisha uhusiano wa wanafunzi na kitabu cha Mwenyezi Mungu.
Amesema kuwa malengo mengine ya masomo hayo ni kufanya juhudi za kuwahamasisha wanafunzi kusoma na kuhifadhi Qur'ani, kuelewa maneno ya Mwenyezi Mungu na kufanyia kazi mafundisho yanayotoa uhai ya Qur'ani Tukufu. 908804