IQNA

Watu wa Ubelgiji kufunzwa ujumbe wa Qur'ani Tukufu

11:49 - January 01, 2012
Habari ID: 2248961
Raia wa mji wa Evere nchini Ubelgiji watafunzwa maarifa ya kitabu kitukufu cha Qur'ani katika kikao kilichopewa jina la 'Hakika na Ujumbe wa Qur'ani Tukufu' kitakachofanyika tarehe 7 Januari.
Maafisa wa Msikiti wa Attauba katika mji wa Evere nchini Ubelgiji wamesema kuwa wameazimia kufanya kikao hicho katika siku za mwanzoni mwa mwaka huu mpya wa Miladia.
Lengo la kikao hicho limetajwa kuwa ni kuarifisha sehemu mbalimbali za kitabu kitakatifu cha Waislamu, Qur'ani kwa raia wasiokuwa Waislamu wa mji wa Evere na wamewaalika wakazi wote wa mji huo kushiriki kwenye kikao hicho.
Maulamaa watakaoshiriki katika kikao hicho wataeleza sababu za kuteremshwa aya za Qur'ani Tukufu, nafasi ya Qur'ani katika maisha ya Waislamu na lengo la kuteremeshwa kwake. 926593
captcha