IQNA

Raia wa Mrekani kupewa zawadi ya nakala ya Qur'ani

17:08 - January 08, 2012
Habari ID: 2253391
Jumuiya ya Waislamu wa kaskazini mwa Marekani ICNA imeanza kugawa nakala za Qur'ani Tukufu na vitabu vya Kiislamu kwa raia mbele ya maktaba za umma kwa shabaha ya kufuta taswira isiyokuwa sahihi ya Wamarekani kuhusu Uislamu na kuarifisha sura halisi ya dini hiyo ya Mwenyezi Mungu.
Muhammad Mudh'hir ambaye ni miongoni mwa maafisa wa jumuiya ta ICNA amesema kuwa kuna fikra potofu na sura isiyokuwa sahihi kuhusu Qur'ani Tukufu katika jamii ya Marekani na kwamba Waislamu wameanzisha ratiba iliyopewa jina la "Kwanini?" kwa lengo la kufuta sura hiyo chafu inayotolewa kuhusu Uislamu.
Mudh'hir ambaye alikuwa akigawa nakala za Qur'ani na vitabu vya Kiislamu mbele ya Makataba ya Umma wa Santa Margarita huko California, amesema lengo la mpango huo ni kuarifisha sura halisi ya Uislamu na Qur'ani kwa sababu aghlabu ya watu wanafananisha utamaduni wa nchi fulani au kundi makhsusi na dini tukufu ya Uislamu. Ameongeza kuwa watu hao wamekuwa wakisikia habari zisizokuwa za kweli katika vyombo vya mawasiliano na kuzinasibisha kwa Uislamu.
Japokuwa hakuna takwimu rasmi kuhusu idadi halisi ya Waislamu nchini Marekani lakini inakadiriwa kuwa ni kati ya watu milioni 6 na 8. 930884


captcha