IQNA

Benki ya Kiislamu yazinduliwa rasmi Tanzania

8:57 - December 02, 2012
1
Habari ID: 2456771
Benki ya kwanza ya Kiislamu Tanzania imezinduliwa rasmi katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
Benki hiyo ijulikanayo kama Benki ya Amana imezinduliwa na Naibu Waziri wa Fedha na Uchumi Tanzania Mh. Saada Mkuya Salum akiwa ameandamana na wakurugenzi wa benki hiyo Dr Idriss Rashid na Bw. Haroon Pirmohamed.
Benki hiyo ambayo imekuwa ikiendesha shughuli zake kwa mwaka mmoja sasa inajivunia kuwa benki ya kwanza kabisa ya Kiislamu nchini Tanzania.
Wakurugenzi wa benki hiyo wanasema lengo kuu la kuanzishwa taasisi hiyo ya kifedha ni kutoa huduma za kibenki za kisasa na za kipekee ambazo zinafuata Sharia za Kiislamu kikamilifu kwa kuzingatia maadili na kwa njia iliyowazi na kwa kutumia teknolojia ya kisasa kwa manufaa ya wateja.
Mbali na akaunti kadhaa za kawaida banki hiyo pia imeanzisha akaunti maalumu ya akiba kwa ajili ya wanaotaka kutekeleza ibada ya Hija.
1145912

Imechapishwa: 1
Inatathminiwa: 0
Haiwezi kuchapishwa: 0
isdory chinyo
0
0
1 : Kwa afsa mikopo, naishi tabora mjini nawezaje kupata mkopo kwenu?,
2 : ni mwenyekiti wa asasi inayosaidia yatima, wagojwa na familia fukara.
Je ! Kuna fungu kwa ajili ya wahitaji?
Kama lipo naomba mawasiliano ya mkuu wa kitengo.
captcha