IQNA

Wamorocco kuishtaki Saudia kuhusu maafa ya Mina

18:33 - October 06, 2015
Habari ID: 3382524
Familia za makumi ya Mahujaji wa Morocco walioaga dunia katika maafa ya Mina karibu na mji mtakatifu wa Makka wamesema wataishtaki serikali ya Saudi Arabia kutokana uzembe uliosababisha kuaga dunia na kutoweka jamaa zao.

Tovuti ya Morocco World News imeripoti kuwa, familia za Wamorocco hao wanashauriana na mawakili waandamizi katika masuala ya kimataifa kwa lengo la kuandaa mashtaka dhidi ya utawala  wa Saudia katika mahakama za kimataifa. Wamorocco hao pia wamehoji kuhusu idadi kubwa ya mahujaji Wamorocco ambao hadi sasa hawajapatikana na kusema suala hilo limeshaanza kufuatiliwa na mawakili wao. Siku ya Ijumaa pia Wamorocco walifanya maandamano kulaani usimamizi mbovu wa  Saudi Arabia katika ibada ya Hija.  Wamorocco wanailaumu serikali ya Saudia kwa kutochukua hatua zozote za maana kuzuia maafa ya Mina. Hatua hiyo ya Wamorocco inachukuliwa huku idadi kubwa ya Waislamu duniani wakiendelea kuikosoa vikali serikali ya Saudia kwa usimamizi wake mbovu katika ibada ya Hija ambapo mwaka huu mnamo Septemba 24 maelfu ya mahujaji wameripotiwa kuaga dunia kufuatia msongamano mkubwa huko Mina.../mh

3382293

captcha