IQNA

Rais wa Iran katika ujumbe wa Ramadhani

Nchi za Kiislamu zishirikiane kukabiliana na misimamo mikali

18:29 - June 07, 2016
Habari ID: 3470366
Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ametoa wito kwa viongozi wa nchi za Kiislamu kushirikiana ili kukabiliana kukabiliana na wale misimamo mikali ya kidini.

Katika ujumbe wake kwa viongozi wa nchi za Kiislamu kwa munasaba wa kuwadia mwezi mtukufu wa Ramadhani, Rais Hassan Rouhani amewataka viongozi wa nchi hizo kuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha kuwa dunia ni pahala salama.

Amesema : "Katika kipindi hiki muhimu kwa historia ya Uislamu, taswira ya kuogofya na bandia ya Uislamu inatishia turathi za kihistoria, falsafa na udugu wa wafuasi wa dini hii tukufu."

Rais Hassan Rouhani amesisitiza kuwa, kuna haja kwa Waislamu wote kuarifisha taswira  halisi na sahihi ya Uislamu na kuudhihirishia ulimwengu kuwa Uislamu ni dini ya amani, huruma na inayohimiza ushirikiano na mshikamano. Rais Rouhani katika ujumbe wake huo ameongeza kuwa, mwezi huu mtukufu wa Ramadhani unatoa fursa na kipindi cha kuunga na kuimarisha udugu miongoni mwa Waislamu. Rais wa Iran ametoa mkono wa kheri na fanaka kwa viongozi wa nchi za Kiislamu, serikali na Waislamu wote kwa munasaba wa kuwadia Mwezi Mtukufu wa Ramadhani

3504496

captcha