IQNA

Uwahhabi ni chanzo cha ugaidi, chuki dhidi ya Uislamu nchini Nigeria

18:51 - October 31, 2017
Habari ID: 3471240
TEHRAN (IQNA)-Itikadi ya Uwahhabi imetajwa kuwa chanzo cha ongezeko la ugaidi na chuki dhidi ya Uislamu Nigeria.
Uwahhabi ni chanzo cha ugaidi, chuki dhidi ya Uislamu nchini NigeriaKwa mujibu wa utafiti uliofanywa na mwandishi wa IQNA nchini Nigeria, duru kadhaa zimedokeza kuwa Uwahhabi ni chanzo cha ugaidi na chuki dhidi ya Uislamu nchini Nigeria. Aidha kutokana Uislamu kuharibiwa jina na itikadi potovu ya Uwahhabi, vijana kadhaa Waislamu waliopata masomo ya juu wanaritadi au kudhoofika katika imani yao kaskazini mashariki mwa Nigeria.

Kwa kuzingatia ukweli kuwa Uislamu ni dini ya amani, uadilifu, mantiki mbali na ni mfumo kamili wa maisha yenye kumeletea mwanadamu ufanisi wa dunia na akhera, iwapo dini hii tukufu itatangazwa kwa njia sahihi, idadi kubwa ya watu wasiokuwa Waislamu watanedelea kuvutiwa na Uislamu.

Uchunguzi uliofanywa pia umebaini kuwa, pamoja na kuwepo chuki dhidi ya Uislamu ambayo imetokana kwa kiasi kikubwa na ugaidi wa kundi la magaidi wa Kiwahhabi wa Boko Haram, kuna idadi kubwa ya Wakristo na viongozi wao wanaoamini kuwa Waislamu waliowengi ni wapenda amani.

Tokea Boko Haram ianzishe uasi wake Nigeria mwaka 2009, watu elfu 20 wamepoteza maisha. Aidha zaidi ya watu milioni mbili wamefanywa wakimbizi kufuatia ugaidi wa Boko Haram.

Neno Boko Haram kwa lugha ya Kihausa lina maana ya 'elimu kutoka nchi za Magharibi ni haramu'. Kundi hilo la Boko Haram ambalo lina ufahamu usio sahihi na potovu kuhusu dini ya Kiislamu, limekuwa likitekeleza hujuma katika maeneo mbalimbali ya Nigeria hasa kaskazini mwa nchi hiyo.

3658646/

captcha