IQNA

Watu 90 wapoteza maisha baada ya hospitali kuteketea moto Iraq, siku tatu za maombolezo zatangazwa

22:30 - July 13, 2021
Habari ID: 3474096
TEHRAN (IQNA)- Wakuu wa Idara ya Afya katika Mkoa wa Dhi Qar nchini Iraq wametangaza kuwa watu wasiopungua 90 wamepoteza maisha kufuata mkasa wa moto katika kitengo cha wagonjwa wa corona katika Hospitali ya Imam Hussein as mjini Nasiriya.

Taarifa zinasema malipuko wa mtungi mkubwa wa oxijeni katika kituo hicho cha matibabu ya corona ndio chanzo cha mtoto huo.

Kufuatia mkasa huo, serikali ya Iraq imetangaa siku tatu za maombolezo ya kitaifa.

Baadhi ya vyombo vya habari Iraq vinasema walioathirika ni wafanyakazi wa sekta ya afya wakiwemo wauguzi na pia maafisa wa zima moto.

Waziri Mkuu wa Iraq Mustafa al Kadhimi amefika katika mji wa Nasiriya kwa ajili ya kufuatialia hali ya mambo baada ya mkasa huo.

Spika wa Bunge la Iraq Mohammad al Hakbousi ameandika katika ukursa wa Twitter kuwa ataitisha kikao cha dhararu leo kwa lengo la kuchunguza maafa hayo ya moto.

Huku ukiwa umeharibiwa na vita na vikwazo, mfumo wa afya wa Iraq umekuwa ukipambana kukabiliana na janga la virusi vya corona ambalo limewaua watu 17,592 na wengine zaidi ya milioni 1.4 wakiwa wameambukizwa.

سه روز عزای عمومی در پی آتش‌سوزی در بیمارستان امام حسین(ع) ناصریه / واکنش مقامات عراقی + فیلم

سه روز عزای عمومی در پی آتش‌سوزی در بیمارستان امام حسین(ع) ناصریه / واکنش مقامات عراقی + فیلم

سه روز عزای عمومی در پی آتش‌سوزی در بیمارستان امام حسین(ع) ناصریه / واکنش مقامات عراقی + فیلم

3983715/

Kishikizo: iraq hospitali moto
captcha