IQNA

Wiki ya Umoja wa Kiislamu

Waislamu wa Kisuni na Kishia wameifanya Iran kuwa imara

16:13 - October 09, 2022
Habari ID: 3475904
TEHRAN (IQNA)- Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran (Bunge) amesema kuwa siri ya ushindi wa nchi hii katika sekta mbalimbali ni kuwepo umoja baina ya Masuni na Mashia na kusisitiza kuwa, Waislamu wa Kisuni na pia wa Kishia waliifanya Iran kuwa imara zaidi na yenye nguvu wakati wa kujihami kutakatifu na katika matukio ya ndani kupitia umoja na dhamira yao thabiti.

Leo Jumapili tarehe 12 Rabiul-Awwal mwaka 1444 Hijria inayosadifiana na Oktoba 9 mwaka 2022 Miladia kwa mujibu wa moja ya riwaya, inatambulika kama siku ya kukumbuka kuzaliwa Muhammad Mustafa SAW Mtume Mtukufu wa Uislamu na hutambulika kama siku ya kuanza Wiki ya Umoja baina ya Waislamu duniani.

Waislamu wa Kisuni husherehekea tarehe 12 na wale wa Kishia tarehe 17 Rabiul -Awwal kama siku ya kuadhimisha mazazi ya Mtume Mtukufu wa Uislamu SAW

Imam Khomeini -Mwenyezi Mungu Amrehemu- Mwasisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ambaye alikuwa mmoja wa wahubiri wa umoja duniani alitumia kipindi cha wiki hii moja ya kuanzia tarehe 12 hadi 17 Rabiul -Awwal kwa ajili ya kudumisha umoja na kukurubiana makundi mbalimbali ya Kiislamu na kukitaja kipindi hiki cha wiki moja kuwa ni Wiki ya Umoja. 

Katika kikao cha leo cha wazi cha bunge, Muhammad Bageri Qalibaf Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran amewapongeza Waislamu wote duniani kwa kuwadia Maulidi ya Mtume Mtukufu wa Uislamu na kuanza Wiki ya Umoja wa Kiislamu.

4090445

captcha