IQNA

Qari wa Senegal akisoma Qur'ani katika Msikiti wa Mtume SAW mjini Madina (+Video)

13:43 - December 25, 2022
Habari ID: 3476301
TEHRAN (IQNA) - Mohammad Al-Hady Toure ni kijana msomaji wa Qur'ani Tukufu kutoka Senegal ambaye ni maarufu katika duru za Qur'ani za nchi hiyo ya Afrika Magharibi

Hivi karibuni alisoma Qur'ani Tukufu katika mkusanyiko wa Mahujaji na waumini wakati wa ziara ya kutembelea Msikiti wa Mtume katika mji mtakatifu wa Madina, Saudi Arabia.

Aliseoma aya za 46-49 za Sura al Kahf katika Qur'ani Tukufu:

" Mali na wana ni pambo la maisha ya dunia. Na mema yanayo bakia ni bora mbele ya Mola wako Mlezi kwa malipo, na bora kwa matumaini.  Na siku tutapo iondoa milima na ukaiona ardhi iwazi, na tukawafufua - wala hatutamwacha hata mmoja kati yao. Na wakahudhurishwa mbele ya Mola wako Mlezi kwa safu (wakaambiwa): Mmetujia kama tulivyo kuumbeni mara ya kwanza! Bali mlidai kwamba hatutakuwekeeni miadi. Na kitawekwa kitabu. Basi utawaona wakosefu wanavyo ogopa kwa yale yaliomo humo. Na watasema: Ole wetu! Kitabu hichi kina nini! Hakiachi dogo wala kubwa ila huliandika? Na watayakuta yote waliyo yatenda yamehudhuria hapo. Na Mola wako Mlezi hamdhulumu yeyote."

captcha