IQNA

Mwanamke wa Algeria aliyehifadhi Qur’ani afariki akiwa na miaka 75

20:49 - September 19, 2024
Habari ID: 3479456
IQNA - Mwanamke wa Algeria ambaye alijifunza Qur’ani Tukufu kwa moyo akiwa na ameaga dunia kutokana na saratani akiwa na umri wa miaka 75.

Rabi’ah Faraq aligundulika kuwa na saratani alipoingia muongo wa 70  wa umri wake lakini Pamoja na hayo aliweza kuhifadhi Qur’an Tukufu  alipokuwa akitibiwa katika hospitali ya Uhispania.

Aliweza kuhifadhi Juzuu 15 akiwa hospitalini na pia wakati huo, licha ya umri wake, aliweza kumaliza masomo yake ya chuo kikuu na kupata shahada ya BA.

Alikuwa akitaka kuhifadhi Quran tangu utotoni, na akiwa na umri wa miaka 75, ndoto yake hatimaye ilitimia.

Qur’ani Tukufu ndio Maandiko pekee ya kidini ambayo wafuasi wake wanaweza kuhifadhi.

Watu wasiohesabika katika kila umma wa Kiislamu wamehifadhi Qur’ani Tukufu tangu siku ya kwanza ilipoteremshwa.

Qur’ani Tukufu ina Juzuu  (sehemu) 30, Sura 114  na aya 6,236.

 

4237393

captcha