IQNA - Qari wa Misri Ahmed al-Sayyid al-Qaytani alishika nafasi ya kwanza katika kategoria ya qiraa au usomaji Katika Mashindano ya Kimataifa ya Qur'ani nchini Uingereza wiki iliyopita.
Mashindano hayo ambayo pia yanajulikana kamaHabib ul-Quran yaliandaliwa katika mji wa Batley huko West Yorkshire, Uingereza, kuanzia Oktoba 31 hadi Novemba 3.
Al-Qaytani, 23, aliwashinda maqari kutoka nchi tofauti kama Morocco, Indonesia, Uingereza, Uhispania, Algeria, Bangladesh na Pakistan na kushinda tuzo ya juu katika kitengo cha qiraa.
Hapo awali alishinda tuzo katika matukio mengine ya kimataifa ya Qur'ani yakiwemo yale ya Iran, Misri na Qatar.
Katika tukio la Qur'ani la Uingereza, alisoma Aya ya 16 hadi 18 ya Surah Hud:
3490594