Mwanasoka huyo wa Morocco alieleza kuwa uamuzi wake ulitokana na imani yake ya Kiislamu, ndiyo maana alikataa kushiriki katika kampeni ya "Rainbow Laces" inayokuzwa na chapa ya Ujerumani, inayolenga kuangazia kile kinacho daiwa eti ni "usawa na kujumuishwa" kwenye EPL. Ukweli ni kuwa ni kampeni chafu ya kuhimiza uhusiano wa watu wa jinsia moja.
Wenzake waliamua kumuunga mkono na pia walijizuia kuvaa koti la Adidas. Manchester United ilitoa taarifa kufafanua msimamo wao juu ya kampeni huku ikisisitiza haki ya wachezaji kutoa maoni yao: "Wachezaji wana haki ya kutoa maoni yao, hasa kuhusu imani yao, na maoni haya wakati mwingine yanaweza kutofautiana na yale ya klabu."
Msimamo wa Mazraoui unaonyesha maadili ya kitamaduni na kidini. Vitendo vya ushoga na usagaji pamoja na ufuska wowote ule husika ni marufuku kabisa katika Uislamu.
Qur'ani Tukufu inalaani vitendo vya ushoga waziwazi na kuvitaja kuwa ni dhambi.
4252281