IQNA

Kadhia ya Palestina

Mahakama Yaiadhibu Klabu ya Ujerumani kwa Kumfukuza Mchezaji 'Batili' kwa Kuiunga Mkono Palestina

10:20 - July 14, 2024
Habari ID: 3479119
Anwar El Ghazi ameshinda kesi dhidi ya klabu ya Ujerumani ya Bundesliga Mainz 05, ambayo ilikatisha kandarasi yake kwa kuunga mkono Palestina, kulingana na ripoti za vyombo vya habari vya Ujerumani.

Mahakama ya Kazi ya Mainz iliamua kwamba taarifa za mchezaji huyo wa Uholanzi ziliangukia ndani ya upeo wa uhuru wa kujieleza na ikaona kufukuzwa kwake "kubatili."

Mahakama iliamuru El Ghazi arejeshwe kazini na aendelee kupokea mshahara wake wa kila mwezi wa €150,000 ($163,500).

Mainz awali ilisimamisha kazi na kisha kuionya El Ghazi mwezi Oktoba kwa kutumia maneno "Kutoka mtoni hadi baharini, Palestina itakuwa huru" kwenye Instagram.

Mchezaji kandanda wa Uholanzi Asimamishwa na Klabu ya Bundesliga kwa Kuisaidia Palestina

Akijibu kusitishwa kwa mkataba wake, El Ghazi aliandika kwenye mtandao wa kijamii wa X: "Simamia kilicho sawa, hata ikiwa inamaanisha kusimama peke yako."

 Aliongeza, "Kupoteza riziki yangu sio kitu ikilinganishwa na kuzimu inayoachiliwa kwa watu wasio na hatia na walio hatarini huko Ukanda wa  Gaza."

 Kabla ya kujiunga na Mainz, El Ghazi alichezea vilabu vya Uholanzi Ajax na PSV Eindhoven, Aston Villa na Everton ya Uingereza, na Lille ya Ufaransa.

 Shirikisho la Soka Duniani FIFA latakiwa Kusimamisha utawala huo katili wa Israel kwa Vita vya Mauaji ya Kimbari huko  Ukanda wa Gaza

Zaidi ya Wapalestina 38,300, wengi wao wakiwa wanawake na watoto, wameuawa na mashambulio ya utawala huo katili wa  Israel dhidi ya Ukanda wa Gaza unaozingirwa tangu  tarehe 7 Oktoba, 2023, mwaka jana. 

Mashambulizi ya kikatili ya Israel yanaendelea licha ya wito wa kimataifa wa kusitisha mapigano.

3489122

captcha