IQNA

Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu

Kama Yesu (AS) angekuwa miongoni mwetu, asingesitasita kupambana na wakandamizaji na mabeberu

14:31 - December 26, 2024
Habari ID: 3479955
IQNA-Ukurasa wa lugha ya Kiingereza wa Ofisi ya Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Ali Khamenei, katika mtandao wa kijamii wa X umechapisha ujumbe wake kwa mnasaba wa kumbukumbu ya kuzaliwa Nabii Isa Masih (AS) ambaye ni maarufu kama Yesu miongoni mwa Wakristo.

Siku ya Jumatano usiku, mtandao wa KHAMENEI.IR ulichapisha ujumbe wa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu kwa lugha ya Kiingereza kama ifuatavyo: “Kama Yesu (as) angekuwa miongoni mwetu hii leo, asingesitasita hata kidogo kupambana na viongozi wakandamizaji na mabeberu wa dunia ya leo, na wala asingestahamili njaa na kulazimishwa kuhama kwa mabilioni ya watu ambao wamesukumwa vitani na madola ya kibeberu.

Jana Jumatano, tarehe 25 Desemba 2024, iliadhimishwa na Wakristo kama sikukuu ya Krismasi ambayo ni maadhimisho ya kuzaliwa Yesu Kristo au Nabii Isa mwana wa Mariam (Amani ya Mwenyezi Mungu Iwe Juu Yake-AS-). 

Katika Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kuna idadi ndogo ya Wakristo ambao wana haki kuabudu na hivyo waoa nao pia huadhimisha siku hii katika miji mbalimbali.

Mtukufu Isa Masih (AS), ambaye ametajwa katika Qur'ani Tukufu kama Ruhullah, ni Mtume wa Mwenyezi Mungu na mwana wa Bibi Maryam (AS).

4256258

Habari zinazohusiana
captcha