IQNA

Wahifadhi wa Qur’ani  wa Iraq wasisitiza kutekeleza mafundisho ya Qur’ani Tukufu  katika Maisha

11:46 - January 29, 2025
Habari ID: 3480113
IQNA – Mwakilishi wa Iraq katika kitengo cha kuhifadhi Qur’ani Tukufu  kwenye Mashindano ya Kimataifa ya Qur’ani  ya 41 ya Iran amesisitiza umuhimu wa kutekeleza mafundisho ya Kitabu Kitakatifu katika maisha ya kila siku.

Musa Akram Nuais aliambia IQNA,  pembeni mwa mashindano hayo kuwa kusoma na kutafakari aya za Qur’ani Tukufu  ni muhimu, na baadaye aya hizo zinapaswa kutekelezwa katika maisha ya kila siku.

Alisema alianza kuhifadhi Qur’ani Tukufu  akiwa na umri wa miaka 8 katika Haram ya Imam Hussein (AS) huko Karbala, na alifanikiwa kuhifadhi Qu’rani  yote akiwa na miaka 13.

Teknolojia Mpya Katika Kuhifadhi Qur’ani Tukufu

Alipoulizwa kuhusu matumizi ya teknolojia mpya na ubunifu katika kuhifadhi Quran Tukufu, alisema kuwa kwa asili, kuhifadhi Quran kunahitaji kuisikiliza na kuirudia mara kwa mara, jambo ambalo linaanzisha mchakato wa kuhifadhi.

"Kwa hakika, matumizi ya nyenzo mpya katika kuhifadhi Qu’rani  yanaweza kuwa na manufaa, lakini bado tunahitaji walimu wenye uzoefu ili kuhakikisha kuwa Quran inahifadhiwa kwa usahihi," aliongeza.

Mchango wa Familia Katika Kuhifadhi Qur’ani 

Nuais pia alieleza jinsi familia yake ilivyomsaidia katika safari yake ya kuhifadhi Qur’ani, akisema:

"Nililelewa katika familia inayozingatia Qur’ani. Ndugu zangu watatu pia ni wahifadhi wa Qur’an, na mama yangu amehifadhi Qur’an yote pia. Niliihifadhi Qur’ani  pamoja nao, na kwa kawaida, mazingira ya familia yetu yaliunga mkono uhifadhi wa Qur’ani Tukufu."

Wasomaji wa Qur’ani Tukufu anaowapenda

Alipoulizwa kuhusu wasomaji maarufu wa Qur’ani aliowachukua kama mifano, alisema:

"Ninasikiliza usomaji wa wasomaji wengi, lakini kwa mfano, ninapendelea usomaji wa  qari mashuhuri wa Misri aliyefariki  Ustadh Minshawi. Miongoni mwa wasomaji wa Iraq, ninafurahia usomaji wa Osama Al-Karbalayi, Maytham al-Tammar, na wengineo."

Maoni Kuhusu Mashindano ya Kimataifa ya Qur’ani Tukufu  ya Iran

Alipozungumzia mashindano ya kimataifa ya Qur’ani  yanayoandaliwa na Iran, alisema kuwa inajulikana wazi kuwa mashindano ya kimataifa ya Qur’ani  yanayoandaliwa na Iran ni miongoni mwa mashindano yenye hadhi kubwa zaidi duniani.

 

"Iran imekuwa ikiandaa mashindano haya ya Qu’rani  kwa zaidi ya miaka 40, ikizingatia sana uteuzi wa washiriki na majaji. Mchakato wa uamuzi na utendaji wa washiriki pia unachunguzwa kwa makini," alisema.

liendelea kusema kuwa mashindano kama haya yana nafasi kubwa katika kuhamasisha kizazi kipya kuhifadhi Qu’rani  na kuwasaidia kufikia viwango vya juu katika uwanja huu.

"Pia yanawahamasisha kutamani kufikia kiwango cha wale wanaoshiriki katika mashindano haya."

ashindano ya Kimataifa ya Qur’ani Tukufu  ya Iran

Wasomaji na wahifadhi wa Qur’ani  kutoka nchi 144 walishiriki katika raundi za awali za Mashindano ya Kimataifa ya Qur’ani  ya 41 ya Iran, na kutoka kwao, wawakilishi kutoka nchi 27 wamefika hatua za fainali katika vipengele vya wanaume na wanawake.

ainali hizo, ambazo zinafanyika katika mji mtakatifu wa Mashhad, kaskazini-mashariki mwa Iran, zitafikia tamati Ijumaa katika hafla ya kufunga ambapo washindi wakuu watatangazwa na kutuzwa.

Mashindano ya Kimataifa ya Qur’ani  ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran huandaliwa kila mwaka na Shirika la Awqaf na Masuala ya Hisani la nchi hiyo.

Lengo lake ni kukuza tamaduni na maadili ya Qur’ani Tukufu  miongoni mwa Waislamu na kuonyesha vipaji vya wasomaji na wahifadhi wa Qur’ani Tukufu.

 

3491642

 

captcha