IQNA

Hujjatul Islam Shahriari Akutana na Spika wa Bunge la Malaysia

15:46 - January 23, 2026
Habari ID: 3481836
IQNA – Katibu Mkuu wa Jukwaa la Kimataifa la Umoja na Kukurubisha Madhehebu za Kiislamu (WFPIST) amekutana na Spika wa Baraza la Wawakilishi la Malaysia.

Kikundi cha wanazuoni wa Kisunni kutoka Iran waliandamana na Hujjatul Islam Hamid Shahriari katika mkutano huo uliofanyika Alhamisi mjini Kuala Lumpur.

Spika wa Bunge la Malaysia, Johari bin Abdul, aliukaribisha ujumbe wa Iran na akasifu uwepo wa pamoja wa wanazuoni wa Kishia na Kisunni kutoka Iran nchini Malaysia, ishara ya juhudi za kuimarisha maelewano ya Kiislamu katika eneo la Asia ya Kusini Mashariki.

Alisema kuwa uwepo huu unaweza kuwasilisha taswira iliyo wazi ya kuishi kwa amani kati ya Waislamu wa Kishia na Kisunni ndani ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kwa watu wa Malaysia na ulimwengu mzima. Kisha aliwasilisha taarifa kuhusu mfumo wa utawala na muundo wa kisiasa wa Malaysia, akieleza namna taasisi zake zinavyofanya kazi katika mazingira ya kijamii na kisiasa ya Asia ya Kusini Mashariki.

The secretary-general of the World Forum for Proximity of Islamic Schools of Thought (WFPIST) met with the Speaker of the Malaysian House of Representatives.

Kwa upande wake, Hujjatul Islam Shahriari alilitambulisha Jukwaa la Kimataifa la Umoja na Kukurubisha Madhehebu za Kiislamu (WFPIST), akifafanua historia ya kuanzishwa kwake pamoja na malengo yake ya kukuza maelewano, mshikamano na mazungumzo ya Kiislamu.

Alitoa shukrani kwa ushiriki hai wa taasisi na mashirika ya Malaysia katika Mkutano wa Umoja wa Ummah wa Kiislamu na Palestina, ulioandaliwa na WFPIST mjini Kuala Lumpur siku ya Jumatano, tukio lililolenga kuimarisha sauti ya pamoja ya Waislamu katika kukabiliana na changamoto za kisiasa na kibinadamu katika eneo la Palestina.

Wanazuoni wa Kisunni wa Iran waliokuwapo katika mkutano huo waliashiria  hali nzuri ya Waislamu wa Kisunni ndani ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, wakibainisha kuwa Waisunni nchini humo wana takribani misikiti 18,000 na shule za kidini 600, idadi inayoonyesha ongezeko kubwa la shughuli za kielimu na kiibada za Kisunni tangu ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya mwaka 1979.

Habari zinazohusiana: 

Walisisitiza kuwa viongozi wa Swala ya Ijumaa na wahubiri wa Kisunni nchini Iran wana uhuru kamili wa kutoa maoni na mitazamo yao, bila kuwepo vizuizi katika jambo hilo, kauli inayolenga kuonyesha sura halisi ya mahusiano ya madhehebu ndani ya Jamhuri ya Kiislamu.

Aidha, walitilia mkazo umakini maalumu wa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu kwa masuala ya Waislamu wa Kisunni, na kuwataka maafisa wa Malaysia kutoathiriwa na propaganda hasi na kampeni za vyombo vya habari vinavyoendeshwa na maadui wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.

4329730

 

Habari zinazohusiana
captcha