IQNA

Wiki ya Umoja wa Kiislamu

Mkutano wa Kimataifa wa Umoja wa Kiislamu wamalizika Tehran

21:26 - September 21, 2024
Habari ID: 3479465
IQNA - Mji mkuu wa Iran wa Tehran ni mwenyeji wa Mkutano wa 38 wa Kimataifa wa Umoja wa Kiislamu, ulioanza Alhamisi asubuhi, Septemba 19, 2024, katika Ukumbi wa Mkutano wa Kimataifa wa mji huo na limemalizika leo jion.

Rais wa Iran Masoud Pezeshkian alikuwa mzungumzaji mkuu katika sherehe za kuzinduliwa kikao hicho.

Kongamano hili hufanyika kila mwaka wakati waWiki ya Umoja wa Kiislamu  kwa mnasaba wa Maulidi au kumbukumbu ya siku ya kuzaliwa Mtume Mtukufu Muhmmad (SAW) na huandaliwa na Jumuiya ya Kimataifa ya Kukurubisha Madhehebu za Kiislamu. Mwaka huu, Palestina ndio mada kuu ya hafla ya mwaka huu.

Kongamano la Umoja wa Kiislamu la mwaka huu limeafanyika chini ya kauli mbiu ya "Ushirikiano wa Kiislamu kwa ajili ya kufikia Maadili ya Pamoja kwa kutilia mkazo Suala la Palestina." Wanazuoni wa Shia na Sunni kutoka Iran na nchi mbalimbali duniani wanashiriki katika mkutano huo.

Kulingana na waandaaji, wageni kutoka nchi 30, ikiwa ni pamoja na Saudi Arabia, Jordan, na UAE, pamoja na Marekani, Urusi, Indonesia, na wengine, wamehudhuria mkutano huo.

Programu zilizopangwa kwa wageni wa kongamano la 38 ni pamoja na kukutana na Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, kutembelea vituo vya sayansi na teknolojia, kutembelea kaburi la Imam Khomeini kusini mwa Tehran, ziara ya Mnara wa Milad  mjini Tehran, na kushiriki Sala ya Ijumaa. 

3489967

Habari zinazohusiana
captcha