mzingiro

IQNA

IQNA – Utawala wa Israel unakabiliwa na ukosoaji wa pamoja usio wa kawaida kutoka Hispania na Brazil baada ya jeshi lake la wanamaji kuwakamata raia wawili wa nchi hizo kutoka katika meli iliyokuwa ikielekea Gaza katika maji ya kimataifa, kitendo ambacho serikali zote mbili zimesema ni kinyume cha wazi cha sheria za kimataifa.
Habari ID: 3482192    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/02

IQNA – Waandaaji wa msafara mkubwa wa kibinadamu wa meli unaoelekea Gaza wamesema kuwa vikosi vya utawala wa Kizayuni wa Israel vimejaribu kuuzuia msafara huo, kwa kuzuia baadhi ya meli katika maji ya kimataifa kwa kutumia ndege zisizo na rubani (drones), kuvuruga mawasiliano na askari waliopanda meli kwa nguvu.
Habari ID: 3482184    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/04/30

IQNA – Msafara wa meli unaojulikana kama Global Sumud Flotilla, unaolenga kuvunja mzingiro uliowekwa na utawala katili wa Israeli dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Gaza, umefika katika maji ya kimataifa karibu na pwani ya Ugiriki.
Habari ID: 3482179    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/04/29

IQNA-Katika hali ambayo, meli ya "Madleen" iliyokuwa imebeba misaada ya kibinadamu ilikuwa imekaribia Gaza, majeshi ya utawala haramu Israel yalishambulia meli hiyo katika hatua iliyotajwa kimataifa kuwa ni uharamia, na kuwateka nyara abiria wake na hivyo kuzuia misaada hiyo kufika Gaza.
Habari ID: 3480818    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/06/10

Kuhifadhi Qur'ani Tukufu
TEHRAN (IQNA) – Katika sherehe katika ardhi ya Palestina ya Ukanda wa Gaza, wahifadhi 143 wa Qur’ani Tukufu wametunukiwa zawadi katika sherehe iliyohudhuriwa na idadi kubwa ya watu na maafisa wa serikali.
Habari ID: 3476011    Tarehe ya kuchapishwa : 2022/10/31

TEHRAN (IQNA)- Kiongozi mwandamizi wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) amesema wananchi wa Palestina wamekaribia sana kuuvunja mzingiro dhidi ya Ukanda wa Gaza uliowekwa na utawala wa Kizayuni wa Israel kwa kushirikiana na Misri tokea mwaka 2007.
Habari ID: 3473968    Tarehe ya kuchapishwa : 2021/06/01

TEHRAN (IQNA) – Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imeupa utawala haramu wa Israel muhula mwa miezi miwili kuhitimisha mzingiro wake wa miaka 12 dhidi ya Ukanda wa Ghaza.
Habari ID: 3473194    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/09/22