IQNA

Wachezaji Waislamu Kombe la Dunia hawataathirika kiafya Mwezi wa Ramadhani

17:09 - June 24, 2014
Habari ID: 1422159
Mjumbe mwandamizi wa Kamati ya Afya ya Shirikisho la Soka Duniani FIFA amesema kuwa, wachezaji Waislamu watakaofunga mwezi mtukufu wa Ramadhani, hawataathirika kiafya wakati wa kuendelea michuano ya kombe la dunia nchini Brazil.

Jiri Dvorak amesema kuwa, Kamati ya Afya ya Fifa imefanya uchunguzi na utafiti wa kina kuhusiana na afya za wachezaji katika mwezi mtukufu wa Ramadhani na kufikia natija hii kwamba, iwapo wachezaji Waislamu watakula vyakula vinavyohitajika, hawatadhoofika kimwili katika mwezi mtukufu wa Ramadhani. Drovak ameongeza kuwa, kamati hiyo imefanya uchunguzi wa kutosha, hivyo hakuna ulazima wowote kwa wachezaji kuingiwa na wasiwasi kutokana na michuano hiyo kuingiliana na mfungo wa mwezi wa Ramadhani. Wakati huohuo, Michel D'Hooghe Mwenyekiti wa Kamati ya Afya ya FIFA amesema kuwa, hakutakuwa na tatizo lolote kwani utaratibu utakuwa kama ule uliofanyika wakati wa michuano ya Olimpiki iliyofanyika 2012 mjini London, Uingereza. Inatarajiwa kwamba, Waislamu wataanza kufunga mwezi mtukufu wa Ramadhani kuanzia siku ya Jumamosi au Jumapili ijayo.

1422049

captcha