IQNA

Mohsen Haji-Hassani Kargar

Ustawi wa Qur'ani Iran ni kutokana na baraka za Kiongozi Muadhamu

10:02 - June 15, 2015
Habari ID: 3314496
Mohsen Haji-Hassani Kargar aliyewakilisha Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na kupata nafasi ya kwanza katika Mashindano ya 57 ya Kimataifa ya Qur'ani ya Malaysia ameashiria nafasi na hadhi ya juu ya qiraa ya Qur'ani Tukufu katika Jamhuri ya Kiislamu.

Haji-Hassani Kargar aliyechukua nafasi ya kwanza katika kitengo cha qiraa cha mashindano  hayo amesema Iran imeweza kupiga katika katika masuala ya Qur'ani kama vile qiraa kutokana na baraka za uongozi wenye busara wa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Sayyid Ali Khamenei ambaye kwa hakika ni Ustadhi mkubwa wa Qur'ani katika Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.


Haji-Hassani Kargar ameyasema hayo katika mahojiano na waandishi habari pembizoni mwa sherehe za kufunga mashindano ya ya Qur'ani nchini Malaysia.
Akijibu swali kuhusu kiwango cha mashindano hayo ya Qur'ani, amepongeza kiwango chake cha juu hasa cha washiriki kutoka Misri, Indonesia na Malaysia.


Mashindano ya 57 ya Kimataifa ya Qur'ani Tukufu ya Malaysia yalianza Jumanne wili iliyopita na kuendelea kwa siku tano kwa kuwaleta pamoja washiriki kutoka nchi 70.../mh

3314383

Habari zinazohusiana
captcha