Kwa mujibu wa tovuti ya al-Sharq, hafla ya kuwaenzi mahufadh hao ilifanyika katika Kituo cha Utamaduni cha Rashad al Shawa huko Ghaza kwa ushirikino wa Taasisi ya Misaada ya Eid ibn Muhammad Al Thani.
Waliohudhuria hafla hiyo ni pamoja na Sheikh Hassan Al-Laham, Mufti wa Ghaza, Sheikh Abdullah ibn Sulayman Al-Misri, Taasisi ya Dar-ul-Qur’an na Sunnah, Sheikh Abdul Basit Al-Satl na maustadh kadhaa wa Qur’ani Tukufu.
Maafisa wa Dar-ul- Qur’an wamewashukuru wote waliounga mkono miradi ya Qur’ani katika kituo hicho.
Eneo la Ghaza limekuwa chini ya mzingiro wa kinyama wa utawala wa Kizayuni kuanzia mwaka 2007. Aidha utawala wa Kizayuni umehujumu kijeshi eneo hilo mara kadhaa ambapo maelfu ya Wapalestina wameuawa shahidi waengi wao wakiwa ni wanwake na watoto. Pamoja na kukumbana na masaibu hayo, Wapalestina katika eneo hilo wamesimama imara kwa imani yao huku wakiendeleza mapambano dhidi ya utawala katili wa Israel.../mh