Kikao hicho imeandaliwa na Shirika la Kiislamu la Elimu, Sayansi na Utamaduni ISESCO na kinatazamiwa kuanza Jumapili tarehe 20 Septemba.
Kwa mujibu wa tovuti ya ISESCO kikao hicho kitajumuisha wakuu wa Vituo vya Kiutamaduni na Jumuiya za Kiislamu kutoka Argentina, Guyana, Ecuador, Mexico, Peru, Venezuela, Chile, Puerto Rico, Columbia, Costa Rica, Jamaica, Trinidad na Tobago, Barbados, Visiwa vya Virgin, Antigua na Barbuda, Grenada, Jamhuri ya Dominican, Visiwa vya Cayman, Saint Martin, Martinique, Turks na Caicos, Bermuda, Suriname, Bahamas, na French Guiana .
Kikao hicho kinalenga kujadili njia za kuimarisha maadili ya Kiislamu miongoni mwa Waislamu katika eneo hilo.
Aidha mkutano huo utajadili mafanikio yaliyopatikana katika kustawisha hali ya Waislamu katika eneo hilo katika fremu ya 'Stratijia ya Utamaduni wa Kiislamu nje ya Nchi za Kiislamu."
Shirika la ISESCO ni chombo cha Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu OIC na hujushughulisha na kama jina lake linavyoashiria, hujishguhulisha masuala ya kiutamaduni, kisayansi na kielimu.../mh