IQNA

Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu

Kuwakamata wanajeshi wa Marekani katika maji ya Iran ni ushujaa

7:22 - January 25, 2016
Habari ID: 3470087
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amepongeza hatua ya hivi karibuni ya Jeshi la Majini la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu IRGC ya kuwakamata wanajeshi wa Marekani walioingia kwenye maji ya Iran kinyume cha sheria.

Ayatullah Ali Khamenei Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema kuwa, hatua hiyo ya kuwakamata wanajeshi wa Marekani walioingia kwenye maji ya Iran kinyume cha sheria katika Ghuba ya Uajemi, ni kitendo cha kishujaa na kilichofanyika kwa wakati unaofaa kabisa.

Ayatullah amesema hayo Jumapili mjini Tehran wakati alipoonana na maafisa wa jeshi la Sepah na sambamba na kuwashukuru wanajeshi hao wa Iran amesema: Kwa hakika inabidi tulihesabu tukio hilo kuwa limefainyika kwa taufiki ya Mwenyezi Mungu ambaye aliwafanya wanajeshi wa Marekani waingie katika maji ya Iran na wanajeshi wetu wachukue hatua ya haraka na ya kishujaa ya kuwatia mbaroni wanajeshi hao na kuwalazimisha kuweka mikono vichwani.

Itakukumbukwa kuwa, boti mbili za Marekani, tarehe 12 Januari 2016 zilikamatwa na wanajeshi wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu Sepah baada ya kuingia kinyume cha sheria katika maji ya Iran na kuwatia mbaroni wanajeshi 10 wa Marekani waliokuwemo kwenye boti hizo.

Wanajeshi hao wa Marekani waliachiliwa huru baada ya kubainika kuwa waliingia kimakosa katika maji ya Iran.

3469911/

captcha