IQNA

Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia atahadharisha

Mgogoro wa Syria unaweza kugeuka kuwa baina ya Sunni na Shia

20:35 - April 28, 2016
Habari ID: 3470277
Russia imetahadharisha kuwa mgogoro was asa nchini Syria huenda ukaibua mgawanyiko mkubwa katika ulimwengu wa Kiislamu.
Akizungumza katika Kikao cha Kimataifa cha Usalama MCIS mjini Moscow hii leo, Sergey Lavrov, Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia amesema kuna hatari ya mgogoro wa kisiasa na kiusalama unaoendelea kushuhudiwa nchini Syria ukageuka na kuwa mpasuko kati Waislamu wa madhehebu ya Shia na Sunni.

Huku hayo yakijiri, maafisa wa Syria wamenasa gari lililokuwa na silaha, yakiwemo makombora, maguruneti na bunduki zilizokuwa na nembo za kuashiria kuwa zimetengenezewa Israel. Shirika rasmi la habari nchini Syria la SANA limeripoti kuwa, dereva wa gari hilo ameuawa katika operesheni hiyo katika mkoa wa Suwayda. Imerifiwa kuwa, silaha hizo zilikuwa zinapelekewa kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh, katika mkoa wa Dara'a.

Hivi karibuni, mjumbe maalumu wa Umoja wa Mataifa katika masuala ya Syria alinukuliwa akisema kuwa, watu wapatao laki nne wamepoteza maisha kutokana na vita vya zaidi ya miaka mitano vilivyoikumba nchi hiyo ya Kiarabu.

3492830

Kishikizo: lavrov iqna shia sunni
captcha