Kwa mujibu wa mwandishi wa IQNA, kampeni hiyo inalenga kuhimiza Amani duniani, udugu wa mataifa na pia kuwazindia Waislamu kuhus uovu wa ugaidi sambamna na kuhimiza moja wa kitaifa, uzalendo na kufikisha ujumbe wa Qur'ani Tukufu kwa walimwengu.
Kampeni hiyo pia inajumuisha maqarii wa kimataifa kutoka Chuo Kikuu cha Al Azhar cha Misri wakiwemo Shaikh Mustafa Abdul Fatah Mohammed Khaleel, Shaikh Abdul Basit Fawzy Ismail, Shaikh Mohammed Mahmood Al-Sayeed, Shaikh Yousuf Akheel na Shaikh Sama Zain. Halikadhalika maqarii wa kimataifa kutoka Saudia, Sudan na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran pia wamealikwa.
Ratiba ya kampeni hiyo inajumuisha qiraa ya Qur'ani Tukufu kote india pamoja na dhifa za futari na maonyesho mbali mbali kuhusu maudhui za kampeni hiyo.
3460055