
Kwa mujibu wa tovuti ya khamenei.ir, katika kumbukumbu ya mwaka wa 47 wa ushindi wa Mapinduzi na mwanzo wa sherehe za 'Afajiri 10', Kiongozi wa Mapinduzi leo asubuhi alifika katika kaburi la Imam Khomeini (rehema za Mungu ziwe juu yake) na kusoma Fatiha kama ishara ya kuheshimu na kuenzi hadhi ya mwanzilishi wa Jamhuri ya Kiislamu.
Ayatullah Khamenei, baada ya kusoma Fatiha na kuswali katika haram ya Imam Khomeini (MA), alimuomba Allah SWT aipe daraja za juu roho ya Imam huyo mkubwa na mpiganaji wa njia ya haki, pamoja na mashahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu.
Kila mwaka, Wairani na wapenda haki kote duniani huadhimisha kumbukumbu ya ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu kuanzia tarehe 1 hadi 11 Februari, ambazo hujulikana kama sherehe za Alfajiri Kumi.
Habari inayohusiana:
Taifa la Iran liliuangusha utawala wa Pahlavi ulioungwa mkono na Marekani miaka 47 iliyopita, na hivyo kumaliza zaidi ya miaka 2,500 ya utawala wa kifalme nchini humo.
Mapinduzi ya Kiislamu yaliyoongozwa na marehemu Imam Khomeini yaliweka mfumo mpya wa kisiasa uliotegemea misingi ya Kiislamu kwa kujumuisha wananchi waliowengi.
3496248