IQNA

Hofu ya Waislamu Uingereza kuhusu Waziri Mkuu mpya

10:17 - July 14, 2016
Habari ID: 3470454
Waislamu nchini Uingereza wamebainisha hofu ya kuhusu kuteuliwa Bi.Theresa May kama Waziri Mkuu kutokana na sera zake haribifu kwa jamii ya Waislamu nchini humo.
Taarifa zinasema May anatazamiwa kuendeleza sera zake dhidi ya Waislamu akiwa katika nafasi ya kiongozi wa Uingereza.
May ambaye aliwahi kuwa waziri wa mambo ya ndani alichukua hatamu za uongozi Uingereza siku ya Jumatano kutoka kwa David Cameron na ameahidi kupambana na kile alichokitaja kuwa ni misimamo mikali kwa kustawisha thamani na mila za Uingereza hasa uhuru wa maoni.
Hii ni haki ambayo aliwapokonya wanachuo Waislamu katika vyuo vikuu vya Uingereza mwezi Novemba mwaka 2014 wakati alipopendekeza Sheria ya Kukabiliana na Ugaidi. Sheria hiyo ambayo ilipitishwa katika bunge la Uingereza iliwazuia wanafunzi Waislamu kubainisha mitazamo yao katika mihadhara na semina kwa hofu ya kutajwa kuwa wenye misimamo mikali. Wakati May akiwa waziri wa mambo ya ndani, Waislamu Uingereza waliandamwa na kupelelelzwa na maafisa maalumu wa polisi waliotumwa katika mitaa yao. Ni kwa sababu hii ndio mwaka jana Tume ya Haki za Binadamu za Kiislamu ikamtaja May kuwa 'Mtu Mwenye Chuki Dhidi ya Uislamu katika Mwaka' au Islamophobe of the Year.
Waislamu Uingereza wanakubaliana kwa kauli moja kuwa, vitendo vya May akiwa Waziri wa Mambo ya Ndani alipelekea chuki na hujuma dhidi ya Waislamu kuwa kitu cha kawaida katika jamii na matokeo yake ni kuwa hali inazidi kuwa mbaya kwa Waislamu milioni tatu nchini Uingereza.
3514951
captcha