IQNA

Morocco yaidhinisha mfumo wa Kiislamu katika benki

10:28 - January 07, 2017
Habari ID: 3470784
IQNA:Morocco imeidhinisha mfumo wa Benki za Kiislamu katika nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika.
Kwa mujibu wa mwandishi wa IQNA, uamuzi huo umechukuliwa ili kwenda sambamba na ongezeko na ustawi wa mfumo kifedha wa Kiislamu katika benki mbali mbali duniani.
Aidha mfumo huo umeanzishwa kama sehemu ya utekeelzwaji wa wa ahadi za chama cha Kiislamu cha Morocco  ambacho kinaongoza serikali ya umoja wa kitaifa ya nchi hiyo.
Baada ya kuingia madarakani chama chenye mielekeo ya Kiislamu na kustawi mfumo wa Benki za Kiislamu, nchi hiyo ya Kiarabu imeonesha hamu kubwa ya kutumia mfumo huo.
Kwa mujibu wa mafundisho ya Kiislamu, kutoa au kupokea riba ni haramu, wakati msingi mkuu wa benki nyingi duniani ni riba katika uendeshaji wake.
Chama cha Uadilifu na Ustawi cha Morocco kiliahidi mwaka 2011 kwamba kitaanzisha Benki za Kiislamu nchini humo.
Inaonekana kuwa, hivi sasa chama hicho kimeamua kuingia kikamilifu kwenye mfumo wa kibenki wa Kiislamu, kwa kuanzisha benki hizo tano za Kiislamu huko Morocco. 
Kati ya benki za Morocco ambazo zinatazamiwa kutumia mfumo wa Kiislamu ni Benki ya Attijariwafa inayofungamana na familia ya kifalme, benki ya serikali ya Banque Centrale Populaire na benki binafsi ya BMCE Bank of Afrika. Benki hizo zote zina hisa katika nchi nyingi za Kiafrika zinazozungumza Kifaransa. Benki zingine za Morocco ambazo zitatumia mfumo wa Kiislamu ni CIH na Credit Agricole du Maroc.

captcha