IQNA

Saudia yatekeleza hujuma ya kijeshi dhidi ya Waislamu wa Kishia nchini humo

0:07 - July 30, 2017
Habari ID: 3471093
TEHRAN (IQNA)-Askari wa utawala wa kiimla na kikabila wa Saudi Arabia wametekeleza hujuma za kijeshi katika makazi ya Waislamu wa madehebu ya Shia ya mji wa Al-Awamiyah, mashariki mwa nchi hiyo.
Habari kutoka Saudia zinaarifu kwamba katika hujuma hiyo ya kinyama askari hao wa Saudia wamewaua kwa kuwapiga risasi Muhsin Allajamy na kijana mwingine mmoja ambao ni wakazi wa mji huo. Kwa mujibu wa duru za habari katika mji huo, mwili wa Allajamy ulichelewa kuokotwa kutoka mahala alipokuwa umelala kutokana na kuendelea ufyatuaji risasi wa muda mrefu wa askari hao.

Aidha nyumba kadhaa zimeharibiwa na nyingine kuchomwa moto na askari hao. Mashuhuda wameeleza kuwa baada ya askari wa Saudia kuwatia mbaroni watu kadhaa na kufyatua kwa muda mrefu mizinga na risasi, walivamia maduka ya mji huo na kupora vyakula na vitu vingine vya thamani madukani. Wakati huo huo magari ya deraya ya utawala huo, yamepelekwa mjini Al-Awamiyah yakiambatana na askari wa usalama ambao wamekuwa wakihusika na hujuma dhidi ya wakazi wa mji huo ambao wengi wao ni Waislamu wa Kishia.

Tokea Mei 10 wanajeshi wa Saudi Arabia walivamia mtaa wa Al Mosara mjini Awamiyah katika wilaya ya Qatif mkoa mashariki mwa nchi hiyo ambapo tokea wakati huo wamewaua watu kadhaa na kuteteteza moto misikiti, nyumba za raia na shule katika mtaa huo. Aghalabu ya wakaazi wa eneo la Mashariki mwa Saudia ni Waislamu wa madhehebu ya Shia na wanakandamizwa na utawala wa ufalme wa Kiwahabbi wa Saudia.

3623419
captcha