Kwa mujibu wa Kituo cha Masuala ya Qur'ani katika Shirika la Wakfu la Iran, vikao hivyo vinfanyika kwa ushirikiano na Wizara ya Afya.
Wasomaji Qur'ani bingwa kama vile Seyed Mohsen Mousavi, Habib Mahkam, Abbas Salimi, Mehdi Gholamnejad na Mojtaba Mohammadbeigi wanashiriki katika vikao vya kusoma Qur'ani katika hospitali na vituo vya tiba.
Mpango huo wa kusoma Qur'ani unalenga kuwapa motisho wafanyakazi wa sekta ya afya ambao wako mstari wa mbele katika vita dhidi ya corona.