Misahafu iliyondolewa katika misikiti yote ya Morocco kama njia ya kuzuia maambukizi ya COVID-19. Sasa wanaharakati wa Morocco wameanzisha kampeni katika mitandao ya kijamii wakitaka Misahafu irejeshwe misikitini.
Abdul Samad Mukhlis, ambaye ni miongoni mwa wanaharakati, anasema misikiti ilifunguliwa miezi kadhaa iliyopita baada ya kupungua maambukizi ya COVID-19 lakini wakuu wa nchi wamezuia Misahafu kurejeshwa jambo ambalo limewanyima waumini fursa ya kusoma Qur'ani Tukufu.
Hivi sasa waumini wanalazimika kusoma aya za Qur'ani kupitia simu zao za mkononi jambo ambalo linawasabishia wengi matatizo ya macho.