IQNA

Turathi za Kiislamu

Urekebishaji wa zaidi ya Kurasa 18,000 za Hati za Kale na Misahafu katika Astan Quds Razavi

17:31 - January 21, 2025
Habari ID: 3480089
IQNA – Wataalamu katika Maktaba, Jumba la Makumbusho, na Kituo cha Nyaraka cha Idara ya Mfawidhi wa Haram ya Imam Ridha (AS) ambayo ni maarufu kama Astan Quds Razavi wamerekebisha kurasa 18,877 za nakala za Qur'ani au Misahafu na hati za kale katika kipindi cha miezi tisa iliyopita, amedokeza Seyyed Ali Tabatabai, mkuu wa urekebishaji wa nyaraka za kitamaduni katika shirika hilo.

Tabatabai alitangaza mafanikio hayo wakati wa mahojiano, akisisitiza utunzaji wa urithi wa kitamaduni kupitia juhudi za kurekebisha kwa umakini.

“Katika kipindi hiki, majalada 174 ya Qur'ani na hati, pamoja na vitabu 57 vya lithografia katika mkusanyiko wa Razavi, vilirekebishwa na timu yetu ya wataalamu,” alisema.

Wigo wa kazi ya urekebishaji pia ulijumuisha kurasa 1,532 za nyaraka za kihistoria, picha za zamani 67, na karatasi tisa za thamani za ngozi. Kwa kuongeza, wataalamu walitenganisha na kurekebisha kurasa 150 zilizohifadhiwa, ambazo zilijumuisha nyaraka za kihistoria kutoka vipindi mbalimbali.

Vilivyorekebishwa ni sehemu ya hazina kubwa iliyohifadhiwa katika haram au kaburi takatifu la Imam Ridha (AS), moja ya taasisi muhimu zaidi za kidini na kitamaduni katika ulimwengu wa Kiislamu, iliyoko Mashhad, Iran.

Juhudi za urekebishaji katika taasisi hiyo ni sehemu ya mpango mpana wa kulinda na kudumisha uadilifu wa nyaraka za kihistoria na za kidini katika mkusanyiko wake, ambazo zinajumuisha moja ya hazina kubwa zaidi za maandiko ya Kiislamu duniani.

3491527

captcha