Matukufu ya Imam Hussein (AS) na Hazrat Abbas (AS) na eneo la kati ya wawili hao, linalojulikana kwa jina la Bain-ul-Haramain yalikuwa yamejaa mahujaji wa kuomboleza Jumanne usiku.
Iraq iliadhimisha Ashura siku ya Jumatano, Julai 17, mwaka 2024, baada ya Ayatollah Mkuu Seyed Ali al-Sistani kutangaza Julai 8, 2024 kama siku ya kwanza ya Muharram.
Katika nchi nyingine nyingi, Waislamu wa Shia waliadhimisha Ashura siku ya Jumanne.
Wafanya Ziyara wanaokusanyika Karbala kuzuru maeneo matakatifu katika hafla hiyo ya kusikitisha wanatoka sehemu mbalimbali za Iraq pamoja na nchi nyinginezo zikiwemo Iran, Lebanon, Pakistan na Bahrain.
Mfawidhi wa madhehebu mawili takatifu wamekusanya uwezo wao wote kuwahudumia wafanya Ziyara.
Maandalizi maalum pia yamefanywa kwa ajili ya ibada ya Rakdha Tuwairaj juu ya Ashura.
Wakati wa Rakdha Tuwairaj, waombolezaji hutembea bila viatu kutoka mji wa Hindya (zamani ukijulikana kama Tuwairaj) karibu na Karbala hadi kwenye madhehebu matukufu ya Imam Hussein (AS) na Hazrat Abbas (AS) huku wakijipiga kichwa na kifua na kisha kuondoka kwenye makaburi.
Ni njia ya kufanya upya utii na matarajio ya Mauaji ya Ashura.
Ibada hiyo imekuwa ikifanyika kila mwaka kwa takriban miaka 140, isipokuwa wakati utawala wa Baath wa dikteta wa zamani Saddam Hussein ulitawala Iraq.
Waislamu wa Shia Ulimwenguni Pote Waadhimisha Ashura kwa Maombolezo ya
Muharram ni mwezi wa kwanza katika kalenda ya mwandamo ya Hijri.
Waislamu wa madhehebu ya Shia na wengine katika sehemu mbali mbali za dunia, kila mwaka katika mwezi wa Muharram hufanya kuomboleza kumbukumbu ya kuuawa shahidi Imam Hussein (AS) na masahaba zake.
Imamu wa tatu wa Shia (AS) ambaye ni Imam Hussein (AS na kikundi kidogo cha wafuasi wake na wanafamilia waliuawa kishahidi na dhalimu wa zama zake - Yazid Bin Muawiya, katika vita vya Karbala katika siku ya kumi ya Muharram (ijulikanayo kama Ashura) mwaka wa 680. AD.