Kuhitimisha Qur’ani au Khatm al-Quran maana yake ni kusoma Qur’ani Tukufu kuanzia mwanzo hadi mwisho.
Zaidi ya wahifadhi 250 wakiwemo wanaume, wanawake na watoto walisoma Qur’ani katika hafla hiyo, kwa mujibu wa gazeti la kila siku la Al-Arabi al-Jadid.
Huu ulikuwa ni mpango wa kwanza wa Qur'ani kama huu kuandaliwa katika Ukingo wa Magharibi.
Washiriki walianza kusoma Quran baada ya sala ya asubuhi na kuhitimisha Magharibi.
Kikao hicho kiliandaliwa na Kamati ya Kuhifadhi Qur'ani ya Nablus, ambayo ina wanachama zaidi ya 500.
Shughuli za Qur'ani hazijapungua katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan licha ya ghasia za walowezi wa Kizayuni wa Israel ambapo takriban kila siku Wazayuni wakipata himaya ya jeshi la utawala huo ghasibu huvamia miji na vijiji.
3489679