iqna

IQNA

TEHRAN (IQNA)-Bunge la Ufilipino limepitisha muswada wa sheria ya kutangaza tarehe mosi Februari kila mwaka kuwa Siku ya Kitaifa ya Hijabu nchini humo.
Habari ID: 3471201    Tarehe ya kuchapishwa : 2017/10/02

TEHRAN (IQNA) Siku ya leo inasadifiana na mwezi 10 Muharram 1439 Hijria, siku ya kukumbuka wakati damu ilipoushinda upanga kwa ushujaa wa Imam Hussein AS na wafuasi wake wachache katika jangwa la Karbla la Iraq ya leo.
Habari ID: 3471200    Tarehe ya kuchapishwa : 2017/10/01

TEHRAN (IQNA)- Waislamu wa madhehebu ya Shia kote duniani wanashiriki katika maadhimisho ya Siku ya Tasu'a, wakifanya maombelezo ya kukumbuka mapambano ya Karbala yaliyopelekea kuuawa shahidi Imam Hussein AS.
Habari ID: 3471199    Tarehe ya kuchapishwa : 2017/09/30

TEHRAN (IQNA)-Msichana mwenye umri wa miaka 10 ataiwakilisha Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Mashindano ya Kimataifa ya Qur'ani Tukufu ya Shaikha Fatima Bint Mubarak ya Umoja wa Falme za Kiarabu, UAE.
Habari ID: 3471198    Tarehe ya kuchapishwa : 2017/09/29

TEHRAN (IQNA)-Polisi katika mkoa wa Xinjiang kaskazini magharibi mwa China wameamuru familia za Waislamu kukabidhi madhihirisho ya kidini hasa nakala za Qur'ani na misala.
Habari ID: 3471197    Tarehe ya kuchapishwa : 2017/09/28

TEHRAN (IQNA)-Mtafiti mmoja nchini Misri amesema mkataba aliofunga Bwana Mtume Muhammad SAW na Wakristo ni hati ya kwanza kuhusiana na kuheshimu dini tofauti duniani.
Habari ID: 3471196    Tarehe ya kuchapishwa : 2017/09/28

TEHRAN (IQNA)- Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, amekwenda katika Msikiti wa Imam Husain AS hapa Tehran na kuusomea Faatiha mwili mtoharifu wa shahid Mohsen Hojaji, aliyeuliwa shahidi na magaidi wa Daesh au ISIS wakati akilinda Haram ya mjukuu wa Bwana Mtume Muhammad SAW, Bibi Zaynab al Kubra AS nchini Syria.
Habari ID: 3471195    Tarehe ya kuchapishwa : 2017/09/27

TEHRAN (IQNA)-Msikiti umeteketezwa moto katika mji wa Orebro kusini mwa Sweden katika tukio ambalo linaaminika kutekelezwa na watu wenye chuki dhidi ya Uislamu.
Habari ID: 3471194    Tarehe ya kuchapishwa : 2017/09/26

TEHRAN (IQNA)-Waziri wa Waqfu na Masuala ya Kiislamu Misri Sheikh Mohamed Mokhtar Gomaa amesema wizara yake itaanzisha shule za Qur’ani katika misikiti yote mikubwa nchini humo.
Habari ID: 3471193    Tarehe ya kuchapishwa : 2017/09/26

TEHRAN (IQNA)- Waislamu wanajumuika katika Msikiti wa Al Ghadir mjini Dar es Salaam nchini Tanzania kwa ajili ya maombolezo ya kuuawa Imam Hussein AS katika mwezi wa Muharram.
Habari ID: 3471192    Tarehe ya kuchapishwa : 2017/09/26

TEHRAN (IQNA)-Watu wenye chuki dhidi ya Uislamu wamemdunga kisu na kumjeruhi daktari Muislamu katika mji wa Manchester nchini Uingereza.
Habari ID: 3471191    Tarehe ya kuchapishwa : 2017/09/25

TEHRAN (IQNA) Jumuiya ya Kiislamu ya Maelewano ya Kitaifa ya Bahrain (Al Wefaq) imelaani hatua ya vikosi vya usalama kuhujumu madhihirisho ya Ashura na kuendelea kuzingirwa nyumba ya mwanazuoni wa Kiislamu Sheikh Issa Qassim.
Habari ID: 3471189    Tarehe ya kuchapishwa : 2017/09/24

Msomi wa Ahul Sunna nchini Lebanon
TEHRAN (IQNA)-Mwanazuoni wa ngazi za juu wa Ahlul Sunna nchini Lebanon amesema mwamko wa Imam Hussein AS dhidi ya utawala wa kiimla na kidhalimu wa Yazid.
Habari ID: 3471188    Tarehe ya kuchapishwa : 2017/09/23

TEHRAN (IQNA)-Waislamu barani Ulaya wanahisi kuongezeka ubaguzi ambapo wawili kati ya watano (asilimia 40) wakisema wamekumbana na ubaguzi wakati wa kutafuta kazi, nyumba au huduma za umma kama vile elimu an matibabu.
Habari ID: 3471186    Tarehe ya kuchapishwa : 2017/09/22

Katika Hotuba Umoja wa Mataifa
TEHRAN (IQNA)-Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amehutubu katika Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa na kuitahadharisha Marekani kuhusu hatua yoyote ya kukiuka mapatano ya nyuklia ya Iran.
Habari ID: 3471185    Tarehe ya kuchapishwa : 2017/09/21

Rais Hassan Rouhani wa Iran
TEHRAN (IQNA)-Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema hali ya Waislamu wa jamii ya Rohingya nchini Myanmar ni ya kusikitisha huku akisisitiza udharura wa kuishinikiza serikali ya Myanmar ili isitishe mauaji ya kimbari na ukandamizaji dhidi ya Waislamu Warohingya.
Habari ID: 3471184    Tarehe ya kuchapishwa : 2017/09/20

TEHRAN (IQNA)-Mama Muirani na watoto wake mapacha wamefanikiwa kuhifadhi Qur’ani kikamilifu.
Habari ID: 3471183    Tarehe ya kuchapishwa : 2017/09/19

TEHRAN (IQNA)-Jeshi la utawala wa Israel limetumia mabuldoza kubomoa nyumba za Wapalestina katika kijiji kimoja kilichoko Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan kusini mashariki mwa mji wa Al-Quds (Jerusalem) unaokaliwa kwa mabavu na utawala huo wa Israel.
Habari ID: 3471182    Tarehe ya kuchapishwa : 2017/09/19

TEHRAN (IQNA)-Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Al-Mustafa SAW kimetangaza kuanza kusajili majina ya wanachuo wa kigeni nchini Iran watakaoshiriki katika Olimpiadi ya 23 ya Kimataifa ya Qur’ani na Hadithi.
Habari ID: 3471181    Tarehe ya kuchapishwa : 2017/09/19

Sayyid Ammar Hakim
TEHRAN (IQNA)- Sayyid Ammar Al-Hakim, kiongozi wa Muungano wa Kitaifa, ambao ni mrengo mkubwa zaidi wa kisiasa nchini Iraq amesema kuna haja ya kutumiwa njia ya mazungumzo kutatua hitilafu zilizopo kuhusu eneo lenye mamlaka ya ndani la Kurdistan nchini humo.
Habari ID: 3471179    Tarehe ya kuchapishwa : 2017/09/18