IQNA

Hotuba ya Sheikh wa Al Azhar katika Kombe la Dunia

12:49 - June 12, 2014
Habari ID: 1416916
Sheikhe mkuu wa Al Azhar Ahmad Tayyib amehutubu katika sherehe za ufunguzi katika sherehe za ufunguzi wa Kombe la Dunia Brazil baadaye hii leo

Kwa mujibu wa gazeti la Al Masri Al Youm, Ubalozi wa  Misri nchini Brazil umesema hotuba iliyorekodiwa ya Sheikh Tayyib ilirushwa hewani  wakati wa sherehe za ufunguzi wa mashindano ya fainali za soka duniani nchini  Brazil.
Sheikh Tayyib aliombwa rasmi na serikali ya Brazil kutoa hotuba katika ufunguzi wa Kombe la Dunia kuhusu wito wa Uislamu wa kuwepo amani katika maeneo mbali mbali mbali duniani.
Hotuba ya Sheikul Azhar iliashiria aya ya 13 ya Surat Hujuraat isemayo "Enyi watu! Hakika Sisi tumekuumbeni kutokana na mwanamume na mwanamke. Na tumekujaalieni kuwa ni mataifa na makabila ili mjuane. Hakika aliye mtukufu zaidi kati yenu kwa Mwenyezi Mungu ni huyo aliye mchamngu zaidi katika nyinyi. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kujua, Mwenye khabari".
 Sheikh Tayyib amesisitiza kuwa Uislamu unapinga machafuko, misimamo mikali na taasubi na kwamba dini hii tukufu inalipa umuhimu suala la kueneza utamaduni wa amani.
1416531

captcha